Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (AS) –ABNA– Iran imesitisha safari ya ujumbe wake kuelekea Geneva, Uswisi, kwa ajili ya duru ya kwanza ya mazungumzo ya nyuklia na Marekani, ikieleza kuwa hali ya usalama katika eneo hilo imezorota kutokana na kuendelea kwa mashambulizi ya kijeshi ya Israel kusini mwa Lebanon.
Maafisa wa Iran wamesema kuwa hakuna mantiki ya kuendelea na mazungumzo wakati mashambulizi yanaendelea, wakisisitiza kwamba kipengele cha kusitisha mapigano tayari kinakiukwa hata kabla ya mazungumzo hayo kuanza rasmi.
Aidha, Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance, ambaye alikuwa anatarajiwa kuongoza ujumbe wa Marekani katika mazungumzo hayo, naye ameripotiwa kusitisha safari yake kufuatia msimamo huo wa Iran.
Mazungumzo hayo yalitarajiwa kufanyika Geneva kwa ushiriki wa maafisa kutoka nchi mbalimbali, yakiwa ni hatua ya kwanza katika utekelezaji wa makubaliano ya hivi karibuni kati ya Iran na Marekani kuhusu masuala ya nyuklia.
Wakati huo huo, mashambulizi ya Israel nchini Lebanon yanaendelea, hali inayoongeza wasiwasi kuhusu athari zake kwa juhudi za kidiplomasia na utulivu wa eneo la Mashariki ya Kati.
Your Comment